Jumatatu, 9 Desemba 2013

Tanzania ya leo


Tanzania imetimiza miaka 52 toka ipate uhuru wake kutoka kwa waingereza walioyoitawala Tanganyika kama ilivyokuwa inajulikana wakati huu  kuanzia mwaka 1918-1961.
Ikiwa ni miaka 52 ya nchi yetu kujitawala yenyewe nashuhudia mambo mbalimbali yanayoonyesha maendeleo japo tupo katika orodha ya nchini zinazoendelea Dunia.
Maendeleo ni hali ya kutoka katika hali duni kuelekea katika hali ambayo ni nzuri iwe kiuchumi,kisiasa na utamaduni.
Wakati tunapata uhuru 1961 nchi yetu ilikuwa ni changa sana kimaendeleo  hata ongezeko la watu lilikuwa ni chini tofauti na sasa ambapo tupo zaidi ya milioni 40.ongezeko hili linafanya uitaji wa masuala mbalimbali ya maendeleo ya jamii yetu kuongezeka.
Katika suala la miundo mbinu ya nchi yetu ilikuwa duni sana lakini sasa tunaweza kushuhudia nchi yetu ikiunganishwa na mikoa mingi kwa kiwango cha rami.
Elimu,shule za msingi na sekondari zimeongeka na kuwezesha jamii kupeleka watoto wao shule ili kukabiliana adui ujinga.
 Elimu ya juu,vyuo vinavyotoa elimu ya juu vimeongezeka ili kusaidia watu kupata elimu ya juu tofauti na kabla ya uhuru vyuo vilivyotegemewa vilikuwa ni vya nje lakini sasa nashuhudia vyuo mbalimbali vikitoa wasomi wa fani tofauti kama wahandisi,walimu,wahasibu,waandishi wa habari  na matabibu na wengine wengi wakiongezeka Tanzania.
Kilimo,najivunia kuona kuwa miaka 52 jamii yetu imeweza kutambua sekta ya kilimo kwa kuanzisha sera ya kilimo kwanza ili kila mtu awajibike katika kilimo ili kujipatia kipato na chakula kwaajili ya kupambana na adui umasikini.
Afya,huduma za afya zimeongezeka sehemu mbalimbali ili jamii iweze kupata huduma ya afya kwa ukaribu.
Biashara,wajasiriamali wameongezeka,jamii imepata muamko wa kufanyabiasha za kitaifa na kimataifa katika kukabiliana na hali ya maisha kulinganisha na nyuma.
Ni mengi ambayo tunaweza kujivunia katika safari yetu ya miaka 52 ya uhuru kama nchi inayoendelea,tuangalie changamoto kama fursa kwetu na kuacha kujilinganisha na nchi nyingine ambazo zimeendelea siku nyingi.Naona Tanzania yetu inakua.
Mung Ibariki Tanzania


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni